Main Article Content

Usawiri wa taswira za ngono katika nyimbo za Bongofleva: mifano kutoka nyimbo teule za WCB


Christopher B. Lucas

Abstract

Nyimbo hizi huakisi masuala mbalimbali katika jamii. Ngono ni suala mojawapo ambalo huakisiwa katika nyimbo za Bongofleva. Aidha, suala la ngono katika jamii za Kiafrika huchukuliwa kuwa jambo la siri na si la kusema hadharani. Hali hii imewafanya wasanii wa Bongofleva kutumia taswira katika kusawiri masuala ya ngono. Hata hivyo, taswira za ngono zinazotumika katika nyimbo za Bongofleva bado hazijulikani kwa sababu hazijatafitiwa na kuwekwa wazi. Kwa hiyo, makala hii imelenga kuchunguza jinsi taswira mbalimbali zinavyosawiri masuala ya kingono katika nyimbo za Bongofleva. Data za makala hii zilikusanywa kutoka katika nyimbo teule za WCB1 kwa kutumia mbinu ya usikilizaji makini na utazamaji wa video za nyimbo teule kutoka katika mtandao wa YouTube. Data hizo zilifafanuliwa na kuchambuliwa kwa kutumia mkabala wa kitaamuli, tukiongozwa na Nadharia ya Semiotiki. Matokeo ya utafiti yameonesha kuwa nyimbo za Bongofleva hutumia taswira mbalimbali za ngono zinazoakisi tendo la ngono na viungo vya ngono. Kwa ujumla, usawiri wa taswira za ngono katika nyimbo za Bongofleva haupaswi kuchukuliwa katika mrengo mmoja tu, yaani hasi, kwani kuna wakati hutumika kutoa elimu ya mahusiano ya kijinsia kwa jamii.


Journal Identifiers


eISSN: 2591-7013
print ISSN: 2665-0789