Kioo cha Lugha https://www.ajol.info/index.php/kcl <p><em>Kioo cha Lugha</em> is an international journal published by the Institute of Kiswahili Studies (IKS). The journal is devoted to the publication of papers on Kiswahili language, linguistics and literature and other African languages. It promotes critical discussions and reviews, especially on contemporary issues regarding language and literature. The journal also publishes short pieces of fiction and poems. It is published annually but from 2021 it will be published bi-annually.</p> <p>Journal website: <a href="https://journals.udsm.ac.tz/index.php/kcl" target="_blank" rel="noopener">https://journals.udsm.ac.tz/index.php/kcl</a></p> <p><br /><br /></p> en-US Copyright is owned by the journal. kidamis@yahoo.com (Dkt. Rhoda Peterson Kidami) leobakize@gmail.com (Dr. Leonard Herman Bakize) Fri, 12 Apr 2024 13:23:49 +0000 OJS 3.3.0.11 http://blogs.law.harvard.edu/tech/rss 60 Dhima ya Miiko katika Uibuaji wa Maudhui katika Fasihi ya Kiswahili: Mifano kutoka Riwaya ya <i>Bw. Myombekere na Bi. Bugonoka Ntulanalwo na Bulihwali</i> https://www.ajol.info/index.php/kcl/article/view/268389 <p>Makala hii inajadili dhima ya miiko katika uibuaji wa maudhui katika fasihi ya Kiswahili. Shabaha kuu ni kubainisha jinsi miiko ilivyo na dhima katika uibuaji wa maudhui mbalimbali katika jamii. Makala hii imetokana na madai ya baadhi ya tafiti zilizotangulia kueleza&nbsp; kwamba miiko ni imani za kishirikina (Frazer, 1940; Smith, 1961; Fielding, 1966) na inatumika katika jamii ambazo ziko nyuma katika&nbsp; masuala ya kisayansi (Madumulla, 1988). Kutokana na mitazamo hiyo, tuliona ipo haja ya kuchunguza dhima ya miiko katika uibuaji wa&nbsp; maudhui kwa wanajamii kupitia riwaya ya Kiswahili. Ili kutimiza azma hii riwaya ya Bw. Myombekere na Bi. Bugonoka Ntulanalwo na&nbsp; Bulihwali ilichunguzwa. Uchambuzi wa data uliongozwa na Nadharia ya Ontolojia ya Kiafrika. Matokeo ya uchunguzi katika makala hii yamebaini kuwa miiko katika fasihi ya Kiswahili ina dhima ya kuelezea maudhui mbalimbali. Baadhi ya maudhui hayo ni maadili, mahusiano ya jamii, afya, imani za kijamii, thamani ya kazi na umuhimu wa kutunza mazingira. Miiko hiyo husawiriwa ndani ya jamii na&nbsp; kuakisi uhalisi wa maisha katika miktadha mbalimbali ya kijamii, kiutamaduni, kijiografia na ulimwengu kwa ujumla.&nbsp;&nbsp;&nbsp;&nbsp;&nbsp;&nbsp;&nbsp;&nbsp;&nbsp;</p> Atupele Kamage, Edith B. Lyimo Copyright (c) 2024 https://www.ajol.info/index.php/kcl/article/view/268389 Fri, 12 Apr 2024 00:00:00 +0000 Matumizi ya Mandhari za Kifasihi Simulizi katika Ujenzi wa Dhamira za Ushairi Andishi: Mifano kutoka Diwani za Muhammed Seif Khatib https://www.ajol.info/index.php/kcl/article/view/268391 <p>Makala hii inakusudia kuchunguza jinsi mandhari za fasihi simulizi zilivyotumika kujenga dhamira katika diwani za Fungate ya Uhuru (1988), Wasakatonge (2003) na Vifaru Weusi (2016). Sababu ya&nbsp; uchunguzi huu ni kwamba mandhari ni kipengele muhimu cha fani&nbsp; katika&nbsp; ujenzi wa kazi za fasihi andishi kama vile riwaya, tamthiliya na&nbsp; hadithi fupi kuliko utanzu wa ushairi. Data za makala hii&nbsp; zilikusanywa&nbsp; kwa kutumia mbinu ya usomaji makini. Nadharia ya Mwitiko wa&nbsp; Msomaji iliyoasisiwa na Wolfgang Iser (1978), Stanley Fish&nbsp; (1980),&nbsp; James Tompkins (1980), Haus Robert Jauss (1982) na Robert Holub&nbsp; (1984) ndiyo iliyoongoza ukusanyaji na uchambuzi wa data za&nbsp; makala hii. Matokeo ya utafiti yanaonesha kuwa kuna matumizi ya mandhari&nbsp; za fasihi simulizi katika kujenga dhamira. Dhamira hizo ni&nbsp; matabaka,&nbsp; ushujaa na ujasiri, ukombozi wa kifikra, kutoheshimu taaluma na uzalendo wa kweli.&nbsp;</p> Baraka Sikuomba, Joviet Bulaya Copyright (c) 2024 https://www.ajol.info/index.php/kcl/article/view/268391 Fri, 12 Apr 2024 00:00:00 +0000 Mdhihiriko wa U-Naijeria katika Video za Nyimbo za Muziki wa Kizazi Kipya nchini Tanzania https://www.ajol.info/index.php/kcl/article/view/268394 <p>Makala hii inajadili mdhihiriko wa U-Naijeria katika video za nyimbo za muziki wa kizazi kipya wa Kiswahili nchini Tanzania. Utafiti wa makala hii uliendeshwa kitaamuli. Makala ilitumia usanifu wa kifenomenolojia, ambapo tafakuri ilikuwa ni kiini katika kuhusisha na kutoa&nbsp; majawabu ya taarifa mbalimbali zilizochunguzwa. Misingi ya Nadharia ya Uhalisia ilitumika katika ukusanyaji na uchambuzi wa data za&nbsp; utafiti wa makala. Katika uainishaji wa matokeo ya utafiti, mdhihiriko wa U-Naijeria katika video za nyimbo za muziki wa kizazi kipya wa&nbsp; Kiswahili nchini Tanzania ulibainika katika vipengele vya mavazi, ala na midundo ya muziki, mitindo ya kiuchezaji, mandhari, utumiwaji wa&nbsp; vifaa vya kijukwaa na matumizi ya lugha. Mwisho, imependekezwa kuwa ni muhimu kwa wasanii wa muziki wa kizazi kipya wa&nbsp; Kiswahili nchini Tanzania kuhusisha vipengele vya utamaduni katika uundaji wa video zao ili kuwezesha ukuzaji wa sanaa, mila, desturi na&nbsp; maadili ya Kitanzania.&nbsp;</p> Gervas A. Kasiga Copyright (c) 2024 https://www.ajol.info/index.php/kcl/article/view/268394 Fri, 12 Apr 2024 00:00:00 +0000 Relevance of the Portrayal of Masculinity in Ebrahim Hussein’s Plays to the Tanzanian and Kenyan Societies https://www.ajol.info/index.php/kcl/article/view/268395 <p>This paper examines the relevance of the portrayal of masculinity in&nbsp; Ebrahim Hussein’s<em> Kinjeketile and Kwenye Ukingo wa Thim</em>, in&nbsp; response to the scholarly need to establish the relevance of the literary&nbsp; portrayal of masculinity in the plays to the Tanzanian and Kenyan&nbsp; societies. The study is qualitative and adopts Butler’s (1990) Gender Performativity Theory and Connell’s (1995) Gender Order&nbsp; Theory that&nbsp; were both used as a framework for reading, analyzing and interpreting&nbsp; characters’ expressions and performances of&nbsp; masculinity in the&nbsp; selected readings. A Constructivist Paradigm was employed, and it&nbsp; comprised of a number of stages, namely&nbsp; identification of the plays as&nbsp; the primary texts, a close reading of the plays and a review of literature&nbsp; on the gendered portrayals in&nbsp; Hussein’s plays. The researcher finally&nbsp; found that the dramatic portrayal of masculinity in Hussein’s&nbsp; <em>Kinjeketile and Kwenye Ukingo wa&nbsp; Thim</em> is realistic and relevant to the&nbsp; Tanzanian and Kenyan societies. Therefore, the present study is very&nbsp; significant since it gives&nbsp; significant knowledge of the reality and&nbsp; relevance of the two dramatic works of art to the Tanzanian and&nbsp; Kenyan societies with regard to&nbsp; the dramatic portrayal of masculinity&nbsp; in them. The study fills the knowledge gap of the relevance of the literary portrayal of the master- servant relationship between&nbsp; Tanganyikans and the Germans from 1890 to 1904 and the famous&nbsp; 1987 Kenyan ‘Otieno case’, and how&nbsp; masculinity was represented both&nbsp; positively and negatively in both cases.&nbsp;</p> Yohana Makeja John Copyright (c) 2024 https://www.ajol.info/index.php/kcl/article/view/268395 Fri, 12 Apr 2024 00:00:00 +0000 Usawiri wa Nduni za Shujaa katika Kisakale cha Munyigumba wa Jamii ya Wahehe https://www.ajol.info/index.php/kcl/article/view/268397 <p>Makala hii inachunguza usawiri wa nduni za shujaa katika Kisakale cha Munyigumba wa jamii ya Wahehe. Watafiti wa masuala ya nduni za shujaa wa Kiafrika wanaeleza kuwa kila jamii ina nduni zake za shujaa zinazotegemea mtazamo, falsafa na utamaduni wa jamii husika. Hivyo, si rahisi kwa jamii zisizo na uhusiano wa karibu kuwa na nduni za shujaa zinazolandana katika hali zote. Kuwapo kwa mitazamo na tamaduni tofautitofauti kunasababisha sifa za shujaa wa jamii moja kuwa tofauti na za shujaa anayepatikana katika jamii nyingine. Hivyo, kilichofanyika katika makala hii ni kubainisha nduni za shujaa wa jamii ya Wahehe ili kufahamu nduni zake. Makala hii imeongozwa na mawazo ya Nadharia ya Ontolojia ya Kiafrika kwa kuwa shujaa anayechunguzwa anatoka katika jamii za kijadi za Kiafrika. Data za makala&nbsp; hii zimekusanywa kwa njia ya usaili na uchambuzi matini kutoka katika vijiji vya Kalenga na Rungemba, Mkoani Iringa. Matokeo ya utafiti&nbsp; wa makala hii yameonesha kuwa shujaa wa jamii ya Wahehe ana nduni mbalimbali zilizothibitika kupitia Kisakale cha Munyigumba.&nbsp; Aidha, imethibitika kuwa, jamii mbalimbali za Kiafrika zina mfanano mkubwa unaosababisha hata mashujaa wake kuwa na nduni&nbsp; zinazofanana kwa kiasi kikubwa.&nbsp;</p> Aneth W. Kasebele Copyright (c) 2024 https://www.ajol.info/index.php/kcl/article/view/268397 Fri, 12 Apr 2024 00:00:00 +0000 Nafasi ya Biashara za Kimataifa katika Kukuza Uzungumzaji wa Kiswahili kwa Wanafunzi wa Shule za Sekondari Nchini Rwanda https://www.ajol.info/index.php/kcl/article/view/268399 <p>Tafiti zinaonesha kwamba lugha ya Kiswahili nchini Rwanda&nbsp; haizungumzwi vizuri kama lugha nyingine zinazofundishwa nchini&nbsp; humo.&nbsp; Ingawa lugha hii haizungumzwi kwa ufasaha, hasa katika shule&nbsp; za sekondari, wanafunzi wanaojifunza katika baadhi ya shule za&nbsp; sekondari wanapata fursa ya kuchangamana na wazungumzaji wa&nbsp; Kiswahili. Wazungumzaji hao ni pamoja na wazazi, jamaa na marafiki wanaofanya biashara za kimataifa za kuvuka mpaka. Jambo hili&nbsp; husaidia sana katika uimarishaji wa Kiswahili miongoni mwa&nbsp; wanafunzi.&nbsp; Makala hii ililenga kutimiza malengo mahususi mawili.&nbsp; Lengo la kwanza lilikuwa kujadili dhana ya biashara za kimataifa za&nbsp; kuvuka&nbsp; mpaka na dhana ya uzungumzaji wa Kiswahili na lengo la pili&nbsp; lilikuwa kubainisha mchango wa biashara za kimataifa za kuvuka&nbsp; mpaka&nbsp; katika uimarishaji wa uzungumzaji wa Kiswahili kwa&nbsp; wanafunzi wa shule za sekondari nchini Rwanda. Utafiti uliongozwa na Nadharia ya&nbsp; Utamaduni Jamii. Mbinu za uchanganuzi wa matini na&nbsp; mahojiano zilitumiwa kukusanya data. Usampulishaji lengwa ulitumiwa kupata&nbsp; sampuli ya utafiti kutoka kwenye shule zilizoteuliwa.&nbsp; Matokeo ya utafiti yameonesha kuwa biashara za kimataifa za kuvuka&nbsp; mpaka zina&nbsp; mchango mkubwa katika uimarishaji wa uzungumzaji wa&nbsp; Kiswahili kwa wanafunzi wa shule za sekondari nchini Rwanda.&nbsp; Isitoshe, utafiti&nbsp; huu umependekeza kuwa walimu wanapaswa kutumia&nbsp; fursa ya biashara za kimataifa za kuvuka mpaka katika uimarishaji wa&nbsp; Kiswahili&nbsp; miongoni mwa wanafunzi wao.&nbsp;</p> Emmanuel Niyirora, Wallace K. Mlaga Copyright (c) 2024 https://www.ajol.info/index.php/kcl/article/view/268399 Fri, 12 Apr 2024 00:00:00 +0000 Uhawilishwaji wa Wakaa wa Kihehe na Athari zake katika Ujifunzaji wa Kiswahili Sanifu kama Lugha ya Pili https://www.ajol.info/index.php/kcl/article/view/268401 <p>Makala hii imechunguza uhawilishwaji wa wakaa wa Kihehe na athari zake katika ujifunzaji wa Kiswahili kama lugha ya pili. Lengo kuu ni kuchunguza namna uhawilishwaji wa wakaa wa Kihehe katika lugha ya Kiswahili unavyoiathiri lugha hiyo. Data zilikusanywa kutoka kwa wajifunzaji wa lugha ya Kiswahili wa jamii ya Wahehe na walimu wa somo la Kiswahili kwa kutumia mbinu za masimulizi ya hadithi na usaili. Uchambuzi wa data uliongozwa na Nadharia ya Usasanyuzi Linganishi. Matokeo ya utafiti huu yameonesha kuwa uhawilishwaji wa&nbsp; wakaa wa Kihehe katika Kiswahili husababisha athari katika lugha hiyo. Athari iliyobainika ni mabadiliko ya matamshi ya maneno mbalimbali ya Kiswahili ambayo husababisha ubadilishaji wa maana msingi za maneno husika. Ili kuondoa au kupunguza athari hiyo, makala hii imependekeza uelimishaji wa jamii za vijijini kuhusu umuhimu wa lugha ya Kiswahili. Pia, serikali iandae walimu wa kutosha&nbsp; ambao ni wabobezi wa kufundisha Kiswahili kama lugha ya pili.&nbsp;&nbsp;</p> Mwaija Ngenzi Copyright (c) 2024 https://www.ajol.info/index.php/kcl/article/view/268401 Fri, 12 Apr 2024 00:00:00 +0000 Matumizi ya Nahau katika Ujarabati wa Mikakati ya Kisintaksia ya Usimbaji wa Fokasi katika Sentensi za Kiswahili https://www.ajol.info/index.php/kcl/article/view/268402 <p>Usimbaji wa fokasi katika sentensi za lugha za Kibantu hufanyika kwa kutumia mikakati mbalimbali ya kimofolojia, kisintaksia au&nbsp; kifonolojia (van der Wal, 2009; Yonenda, 2011; Morimoto, 2014; Ndumiwe,&nbsp; 2023). Aidha, kuna mbinu tofautitofauti zinazotumika&nbsp; kung’amua&nbsp; ikiwa mikakati madhukura inasimba fokasi au la. Mojawapo ya mbinu&nbsp; hizo ni matumizi ya nahau. Van der Wal (2016, 2021)&nbsp; alichunguza&nbsp; mbinu hiyo katika ung’amuzi wa usimbaji wa fokasi katika lugha za&nbsp; Kimakua (P31), Kizulu (S42), Kimatengo (N13), Kirundi&nbsp; (JD62),&nbsp; Kichangana (S53), Kiganda (JE15), Kinyakyusa (M31), Kibukusu&nbsp; (JD31c) na Kitharaka (E54). Hata hivyo, hakuna utafiti uliofanyika&nbsp; katika lugha ya Kiswahili (G42) kuhusu matumizi ya nahau katika&nbsp; ujarabati wa mikakati ya usimbaji wa fokasi. Kwa hiyo, lengo la&nbsp; makala&nbsp; hii ni kuhakiki mikakati ya kisintakisa ya usimbaji wa fokasi&nbsp; kwa kutumia nahau za Kiswahili. Data zimekusanywa kwa kutumia&nbsp; mbinu za&nbsp; usaili na upitiaji wa nyaraka. Data hizo zimechambuliwa&nbsp; kitaamuli kwa kuongozwa na Nadharia ya Vibadala vya Kisemantiki&nbsp; (Rooth,&nbsp; 2016). Utafiti huu umebainisha kuwa nahau za Kiswahili&nbsp; zikiundiwa sentensi kwa kutumia mikakati ya ukasimishaji, upinduzi&nbsp; wa&nbsp; viambajengo na utenguaji kushoto, maana ya nahau inatoweka.&nbsp; Kwa hiyo, utowekaji wa maana ya nahau huthibitisha kuwa mikakati&nbsp;&nbsp;&nbsp; husika hutumika kusimba fokasi katika lugha ya Kiswahili.</p> Elishafati J. Ndumiwe, Amani Lusekelo Copyright (c) 2024 https://www.ajol.info/index.php/kcl/article/view/268402 Fri, 12 Apr 2024 00:00:00 +0000 Examining the Communicative Value of Sign X in the Public Space in Tanzania: The Case of Swahili Context https://www.ajol.info/index.php/kcl/article/view/268403 <p>This paper investigates the multifaceted communicative value of sign X in the Swahili context in Tanzania, encompassing both physical&nbsp; and virtual spaces. Cities around us are marked by many semiotic signs which present different communication cues and experiences.&nbsp; These signs are imagery symbols which are assigned meaning by the people who use them to communicate different concepts, ideas,&nbsp; beliefs and experiences. To dissect the diverse connotations associated with sign X as it operates within Tanzania’s Swahili context, this&nbsp; study used two distinct datasets: narrative data sourced from survey questionnaires completed by a cohort of 103 participants and&nbsp; collection of 47 photographic data featuring sign X that were captured through digital camera across the physical and virtual public&nbsp; spaces. The study employed Socio-Semiotic Theory to analyse the communicative value of sign X in the studied public space. The theory&nbsp; focuses on how meanings are constructed and communicated through various signs and symbols within Swahili context in Tanzania. The&nbsp; study findings revealed that sign X was employed to communicate multiple meanings in the Swahili context. These include warnings,&nbsp; prohibitions, calls for demolition, removal instructions, misinformation and fake news, cancellations, deletions, hidden value, protocols to&nbsp; observe, marker of death, expression of love and sexuality, and poignant reminders of personal experiences from the past.&nbsp;&nbsp;&nbsp;&nbsp;&nbsp;&nbsp;</p> Paschal C. Mdukula Copyright (c) 2024 https://www.ajol.info/index.php/kcl/article/view/268403 Fri, 12 Apr 2024 00:00:00 +0000