Main Article Content

Matatizo ya Tafsiri katika Matini za Kitalii Nchini Tanzania


Hadija Jilala

Abstract

Utalii ni miongoni mwa sekta muhimu sana katika maendeleo ya nchi na ni sekta ambayo huliingizia taifa pato la kiuchumi. Sekta hii huhusisha watu wa jamii mbalimbali duniani, watu wenye tofauti za kiutamaduni, kiuchumi, kiitikadi, kijamii na wanaozungumza lugha tofauti. Pamoja na hayo, utalii ni eneo ambalo bado halijafanyiwa kazi vya kutosha na watafiti wa lugha na tafsiri ili kuona ni jinsi gani lugha na tafsiri vina mchango katika ukuzaji wa sekta ya utalii nchini Tanzania. Makala haya basi yanachunguza matatizo ya tafsiri katika matini za kitalii zilizotafsiriwa kutoka Kiswahili kwenda Kiingereza. Lengo ni kubainisha matatizo ya tafsiri katika matini za kitalii na kutoa mapendekezo ya namna ya kuyakabili matatizo hayo ili kuleta ufanisi wa mawasiliano.

Journal Identifiers


eISSN: 0856-552X
print ISSN: 0856-552X