Main Article Content

Matumizi ya Mandhari za Kifasihi Simulizi katika Ujenzi wa Dhamira za Ushairi Andishi: Mifano kutoka Diwani za Muhammed Seif Khatib


Baraka Sikuomba
Joviet Bulaya

Abstract

Makala hii inakusudia kuchunguza jinsi mandhari za fasihi simulizi zilivyotumika kujenga dhamira katika diwani za Fungate ya Uhuru (1988), Wasakatonge (2003) na Vifaru Weusi (2016). Sababu ya  uchunguzi huu ni kwamba mandhari ni kipengele muhimu cha fani  katika  ujenzi wa kazi za fasihi andishi kama vile riwaya, tamthiliya na  hadithi fupi kuliko utanzu wa ushairi. Data za makala hii  zilikusanywa  kwa kutumia mbinu ya usomaji makini. Nadharia ya Mwitiko wa  Msomaji iliyoasisiwa na Wolfgang Iser (1978), Stanley Fish  (1980),  James Tompkins (1980), Haus Robert Jauss (1982) na Robert Holub  (1984) ndiyo iliyoongoza ukusanyaji na uchambuzi wa data za  makala hii. Matokeo ya utafiti yanaonesha kuwa kuna matumizi ya mandhari  za fasihi simulizi katika kujenga dhamira. Dhamira hizo ni  matabaka,  ushujaa na ujasiri, ukombozi wa kifikra, kutoheshimu taaluma na uzalendo wa kweli. 


Journal Identifiers


eISSN: 0856-552X
print ISSN: 0856-552X