Main Article Content

Mdhihiriko wa U-Naijeria katika Video za Nyimbo za Muziki wa Kizazi Kipya nchini Tanzania


Gervas A. Kasiga

Abstract

Makala hii inajadili mdhihiriko wa U-Naijeria katika video za nyimbo za muziki wa kizazi kipya wa Kiswahili nchini Tanzania. Utafiti wa makala hii uliendeshwa kitaamuli. Makala ilitumia usanifu wa kifenomenolojia, ambapo tafakuri ilikuwa ni kiini katika kuhusisha na kutoa  majawabu ya taarifa mbalimbali zilizochunguzwa. Misingi ya Nadharia ya Uhalisia ilitumika katika ukusanyaji na uchambuzi wa data za  utafiti wa makala. Katika uainishaji wa matokeo ya utafiti, mdhihiriko wa U-Naijeria katika video za nyimbo za muziki wa kizazi kipya wa  Kiswahili nchini Tanzania ulibainika katika vipengele vya mavazi, ala na midundo ya muziki, mitindo ya kiuchezaji, mandhari, utumiwaji wa  vifaa vya kijukwaa na matumizi ya lugha. Mwisho, imependekezwa kuwa ni muhimu kwa wasanii wa muziki wa kizazi kipya wa  Kiswahili nchini Tanzania kuhusisha vipengele vya utamaduni katika uundaji wa video zao ili kuwezesha ukuzaji wa sanaa, mila, desturi na  maadili ya Kitanzania. 


Journal Identifiers


eISSN: 0856-552X
print ISSN: 0856-552X