Jarida la Chama cha Lugha na Fasihi ya Kiswahili Tanzania (CHALUFAKITA) linamilikiwa na chama hicho ambacho makao makuu yake ni Dodoma,Tanzania. Jarida la CHALUFAKITA lilianzishwa na kusajiliwa tarehe 18/01/2018. Hili ni jarida la kimataifa linalochapisha makala zake mara moja kwa mwaka. Jarida linapatikana katika nakala ngumu pamoja na nakala tepe/mkondoni. Jarida hili limesajiliwa pia na African Journals Online (AJOL). Lengo la Jarida ni kuendeleza na kudumisha lugha ya Kiswahili na utamaduni wa Waswahili. Pia, linalenga kuwajengea uwezo wanataaluma katika kufanya tafiti na kuandika makala mbalimbali zitakazochangia maarifa mapya katika nyuga mbalimbali za lugha ya Kiswahili. Kwa hiyo, tunakaribisha makala kutoka pande zote za dunia zinazohusu Isimu ya Kiswahili, fasihi ya Kiswahili na utamaduni wa Mswahili.

 

Chama cha Lugha na Fasihi ya Kiswahili Tanzania (CHALUFAKITA) Journal is owned by the stated association which is based in Tanzania; and its headquarter is in Dodoma region.  CHALUFAKITA is an international journal which publishes its articles once a year. The Journal can be accessed online and a hard copy is also available. The Journal has also been registered on African Journals Online (AJOL). The main objective of CHALUFAKITA Journal is to develop and promote Kiswahili language and the Swahili culture. The Journal provides an avenue to scholars to undertake research and publish diverse papers that will contribute to knowledge in various disciplines. Therefore, we invite scholars from all parts of the world to contribute scholarly papers which address Kiswahili language in all categories: linguistics, sociolinguistics, literature and culture.

Other websites associated with this journal: https://chaukidu.org/chalufakita

View All Issues

Journal Identifiers


eISSN: 2591-7013
print ISSN: 2665-0789